Katibu
Tawala wa Mkoa wa Tanga, Mhe.Salum Mohammed Chima,leo, Alhamisi, tarehe
13, 2014, amefungua rasmi maadhimisho ya Kitaifa ya Haki za Mlaji kwa
mwaka 2014,
katika viwanja vya Polisi Mabawa, jijini Tanga, huku akiyataka Mabaraza
yanayojishughulisha na Utetezi wa Mlaji kuhakikisha kuwa yanaongeza
utoaji wa
elimu kwa wananchi ili waweze kujua haki na wajibu wao na kuweza kujua
namna
wanavyoweza kuhudumiwa na mabaraza hayo katika kutanzua kero
wanazokabiliana
nazo wakiwa sokoni.
Ufunguzi
huo uliambatana na mdahalo wa wazi la siku moja lililohusisha wanafunzi
zaidi ya 200 kutoka Vyuo na Shule za Sekondari zilizopo Mkoani Tanga.
Vyuo vilivohusika katika kongamano hilo ni pamoja na Chuo cha Biashara
cha Mtakatifu Joseph na Chuo Kikuu cha Eckenforde. Shule zilizoshiriki
ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Popatlal, Shule ya Sekondari ya Mikanjuni na
Shule ya Sekondari ya Usagara. Majadiliano katika mdahalo huo wa wazi
yalijikita zaidi katika huduma zinazodhibitiwa na SUMATRA hususan
usafirishaji wa abiria mijini, maarufu kama usafiri wa Daladala,
udhibiti wa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi, athari za bidhaa
bandia, haki za mlaji au mtumiaji na udhibiti wa huduma za majisafi.
Maadhimisho ya Siku
ya Kimataifa ya Haki za Mlaji, yaliyoanza jana katika viwanja vya Tropicana,
eneo la Mabawa, jijini Tanga, yameandaliwa na kuratibiwa na Jukwaa la Watumiaji (Tanzania
Consumer Forum). Maonesho hayo yatafanyika kwa siku nne katika viwanja hivyo
vya Tropicana, Mabawa, kuanzia Machi 12 hadi 15, 2014, siku ambayo ndiyo kilele
cha maadhimisho ya Haki za Mlaji.
Katika maonesho hayo, wananchi wa
Jiji la Tanga wanapata fursa ya kujifunza kuhusu shughuli zinazofanywa na
Mabaraza ya Ushauri kwa Walaji wa Huduma zinazodhibitiwa na zisizodhibitiwa na Mamlaka
za Udhibiti kwa mashirika ya huduma na miundombinu. Aidha walijifunza shughuli za Tume ya Ushindani.
Tume ya Ushindani na Asasi isiyo
ya Kiserikali ya “Sauti ya Mtumiaji” ni taasisi mbioi zisizo wadhibiti
zilizoshiriki katika maonesho hayo. Washiriki kutoka kwa Mamlaka za Udhibiti ni
pamoja na Mabaraza ya Ushauri kwa Walaji wa Huduma zinazodhibitiwa na SUMATRA,
EWURA na TCRA. Aidha, Baraza la Ushauri kwa Walaji wa Huduma zinazosimamiwa na TCAA
pia lilishiriki katika maonesho hayo.
Kaulimbiu ya maadhimisho hayo kwa
mwaka 2014 inasema “Haki za Mtumiaji wa Simu Zilindwe”. Kaulimbiu hii inalenga
kukumbusha mamlaka husika na kampuni za simu kuhakikisha kuwa zinazingatia haki
za walaji au watumiaji wa huduma za simu kwa kuondoa kero na kuwezesha matumizi
hayo kuwa ya tija zaidi.
Katika banda la Tume la Ushindani, wananchi waliweza kujifunza kuhusu Haki na Wajibu wa Mlaji, Jinsi ya Kutambua Bidhaa Bandia na namna Tume hiyo inavyoendesha shughuli zake kwa ujumla.
Katika banda la Tume la Ushindani, wananchi waliweza kujifunza kuhusu Haki na Wajibu wa Mlaji, Jinsi ya Kutambua Bidhaa Bandia na namna Tume hiyo inavyoendesha shughuli zake kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment