Tuesday 22 April 2014

Taarifa kwa Vyombo vya habari Kuhusu Zoezi la Kaguzi za Kushitukiza Kudhibiti Bindaa bandia Mwanza na Arusha


FCC Yakamata Bidhaa Bandia za Sh. Mil 30/- Mwanza na Arusha

Wakaguzi wa Tume ya Ushindani (FCC), wakifanya kazi kwa mujibu wa Sheria ya Alama za Bidhaa (1963), iliyorekebishwa, pamoja na kanuni za Sheria hiyo za mwaka 2012, wameendesha zoezi la kaguzi za kushitukiza katika miji ya Arusha na Mwanza kati ya Aprili 8 na 12 na kukamata bidhaa bandia zenye thamani ya Sh. Milioni 30/-.

Bidhaa zilizokamatwa katika kaguzi za kushitukiza jiini Mwanza ni kama ilivyoainishwa hapa chini:

Na.
Duka/Mmiliki
Bidhaa Bandia Zilizokamatwa
Eneo
1
M/S Shaban Hussein Kombe (S.K Mobile Phone Shop)
Simu bandia aina ya Tecno mobile (216pcs)  na betri zake (2,556)
Mtaa wa Msikiti Wa Ijumaa
2
Duka la M/S Yassin Ibrahim Nyaludibha
Baygon (12pcs)
Mtaa wa Liberty
3
M/S Mama Mwijage Mini Super Market
Baygon (1pc) na kiwi (1pc)
Mtaa wa Liberty
4
Duka la Patric
Baygon (1pc)
Mtaa wa Liberty
5
M/S Sammiyya Najib Zaharo Mini Super Market
Baygon (1pc)
Mtaa wa Liberty

Operesheni iliyofanyika jijini Mwanza ilihusisha pia ukamataji wa bidhaa bandia za vipodozi 494 vilivyopigwa marufuku. Bidhaa hizo zilikabidhiwa kwa mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Kanda ya Ziwa kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria. Vipodozi hivyo ni pamoja na  Carolight (190pcs), Losheni ya Betasol na krimu yake ya carl (188), Krimu ya Diproson (20 pcs) Losheni ya Diproson (12 pcs), Cocoderm (18 pcs)  na Prolight (18 pcs). Vipodozi vyote vilipatikana katika duka la Bw. Yassin Ibrahim Nyaludibha.

Maduka mengine ambayo yalikaguliwa lakini hayakukutwa na bidhaa bandia ni pamoja na Iman Shop, Lake Printing Works Ltd., Sahara Shop, George Mwendeshe Lukoninga, Joyce Kwandu Kichiba, Emmanuel Joseph Sisha, Abogast Marko Mhalagani, Aron Kisasa Shop na Dunia Mashala Ng’wanaomu.

Aidha, operesheni ya kaguzi zilizoendeshwa jijini Arusha pia iliwezesha kukamatwa kwa bidhaa bandia kama ilivyoainishwa hapa chini:

Na.
Duka/Mmiliki
Bidhaa Bandia Zilizokamatwa
Eneo
1
Highland Hardware
Lorenzetti heater 1pc
Mtaa wa Sokoine
2
 Baltazari Mallya
Lorenzetti heater 3pcs
Mtaa wa Sokoine
3
 CBK trading

Lorenzetti heater  40pcs
Uwanja wa Sheikh Amri Abeid
4
Angelika Quality store
Lorenzetti heater 2pcs
Mtaa wa Levolusi
5
Maria Inocent Massawe
Losheni za Nivea (1pc)

6
Baraka Mangaro Nkya
Losheni za Nivea (11pcs)
Mtaa wa Annex
7
Shamika Enterprises
Losheni za Nivea (28pcs)
Mtaa wa Kaloleni
8
Super Cosmetics
Losheni za Nivea (56 pcs)

9
Janet Cosmetics
Losheni za Nivea (34 pcs)

10
Felix O Kimario
Mafuta ya kulainisha midomo ya Nivea (lip shine) (5 pcs)
Mtaa wa Levolosi
11
Raymond Cosmetics
Losheni za Nivea (28pcs)
Mtaa wa Zaramo

Karibu watuhumiwa wote walitimiza masharti ya utaratibu wa Mkondo wa haraka wa utanzuaji mashauri kwa mujibu wa Sheria ya Alama za Bidhaa (offence compoundment procedure) na kulipa faini kwa mujibu wa taratibu na kanuni za sheria hiyo, wakati bidhaa walizokamatwa nazo zikisubiri kuteketezwa.

Hata hivyo, mtuhumiwa mmoja, M/S Shamika Enterprises, alieleza dhamira yake ya kutumia mkondo wa mahakama za kawaida kupinga utaratibu wa adhabu uliotumiwa na Mkaguzi Mkuu wa MMA katika kumuadhibu. Shauri hilo litafuata Mkondo wa Sheria ya Makosa ya jinai kama ilivyoainishwa katika Sheria husika.

Kaguzi zote ziliendeshwa kwa kushirikiana na wasimamizi na wawakilishi wa wamiliki wa hataza na miliki bunifu zilizobainika kughushiwa katika bidhaa zilizokamatwa, pamoja na maafisa wa jeshi la polisi.

Wakaguzi wa FCC pia waliendesha kaguzi katika maduka manne ya mauzo ya jumla na reja reja ya betri za Tiger Head mnano tarehe 9 Aprili, 2014. Maduka hayo ni pamoja na Neema Investment, Duka la Nancy, Duka la Mtei, na duka la Setway pamoja na maghala yanliyoshukiwa kuhusiana na maduka hayo katika maeneo ya Unga Limited, Moromboo na Mbauda. Maduka na ghala hizo hayakukutwa na bidhaa bandia za Tiger Head zilizohofiwa kuhodhiwa humo.

Hatua hiyo ni mwendelezo wa juhudi za Tume zilizofanywa na tume za kufanya kaguzi za kawaida pamoja na kaguzi nyingine 7 za kushitukiza katika maduka na bohari zinazomilikiwa na watu binafsi, ambazo zinahofiwa kuhodhi bidhaa bandia, baina ya Julai 1, 2013 na Aprili 11, 2014 katika mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam. Operesheni hizo ziliwezesha kukamatwa kwa bidhaa bandia ikiwa ni pamoja na makontena 240 yaliyokuwa na shehena za bidhaa bandia zenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 200/- na wafanyabiashara wapatao a71 kuadhibiwa kwa kukiuka Sheria ya Alama za Bidhaa. Baadhi ya bidhaa zilizokamatwa katika operesheni hizo za awali ni pamoja na Simu bandia za Samsung, NOKIA and TECNO zaidi ya 400, Mabomba 738 ya maji ya IPS, Vifaa vya michezo 1,248 vya Klabu ya Mpira ya Simba, Vyandarua za kuzuia mbu, Vifaa 1,166 vya umeme vya Phillips, Pakiti 12,053 za nyembe bandia za Gillette na Swichi za Umeme aina ya MEM zipatazo 19.

Operesheni za kaguzi za kushitukiza katika maeneo yote yanayohofiwa kuhodhi bidhaa bandia ni zoezi endelevu na linaendeshwa kote nchini likilenga kuwakamata na kuwafikisha katika mkono wa sheria wahalifu wote wanaojishughulisha na biashara ya bidhaa bandia. Kusjishughulisha na biashara ya bidhaa bandia kunawaathiri wamiliki hataza na miliki bunifu, kuaathiri uchumi na kunakiuka haki za walaji nchini.
Imetolewa na Mkaguzi Mkuu wa Sheria ya Alama za Bidhaa

MKAGUZI MKUU, SHERIA YA ALAMA ZA BIDHAA
Aprili 22, 2014

No comments:

Post a Comment