
This Blog keeps you abreast key events relating to the Fair Competition Commission. The Commission was established by the Fair Competition Act (No. 8 of 2003) to promote and protect effective competition in Trade and Commerce and to protect consumers from misleading and deceptive conducts. It also fights counterfeits under the Merchandise Marks Act (1963) as amended.
Wednesday, 6 December 2017
Hotuba ya Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Mhandisi Stella Martin Manyanya (MB) akifungua Maadhimisho ya Siku ya Ushindani Duniani na Semina kwa Wadau wa Sheria ya Ushindani, GEPF House, Dar es Salaam, Desemba 5, 2017
HOTUBA
YA MGENI RASMI, NAIBU WAZIRI WA VIWANDA,
BIASHARA NA UWEKEZAJI, MHESHIMIWA MHANDISI STELLA MARTIN MANYANYA (MB), KATIKA UFUNGUZI WA SEMINA KWA WADAU WA SHERIA YA USHINDANI TAREHE
05 DESEMBA, 2017 KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA GEPF
Mwenyekiti
wa Tume ya Ushindani - Prof. Samweli
Wangwe,
Makamishna
wa Tume ya Ushindani - Mr. Felix Kibodya na Mr. Fadhili Manongi
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu Tume ya Ushindani -Dkt.
John Mduma
Menejimenti
ya Tume ya Ushindani
Wawakilishi
kutoka Wizara, Idara na
Taasisi
za Serikali zilizopo hapa,
Viongozi
wa Mashirikisho, Vyama na Jumuiya za Wazalishaji na Wafanyabiashara,
Wafanyabiashara
mliohudhuria,
Wawezeshaji
kutoka Tume ya Ushindani na Taasisi nyingine za Serikali,
Waandishi
wa Habari,
Mabibi
na Mabwana,
Itifaki
Imezingatiwa
Habari
za asubuhi,
"Awamu ya Mhe. Dkt. John Pombe
Joseph Magufuli ni ya Uchumi wa Viwanda."
Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii
adhimu kuwakaribisha washiriki wa kikao kazi hiki kinachojumuisha Mamlaka za
Udhibiti, vyama vya wafanyabiashara, wazalishaji na wanahabari.
Leo ni siku ya kipekee ulimwenguni. Ni siku
ya Kimataifa ya Ushindani. Siku hii ni muhimu kwetu watendaji wa Serikali na
wafanyabiashara pia. Ni siku tunayokumbushana majukumu yetu ya pamoja katika
kuendesha uchumi kwa namna inayoleta na kuhakikisha ustawi endelevu katika
biashara, uchumi na maslahi ya mlaji ambaye ndiye mteja.
Umuhimu wa kipekee wa siku hii unatokana na
ukweli kuwa kwa sasa dunia imekuwa kama kijiji, maendeleo ya Sayansi na
Teknolojia yanawezesha taarifa mbalimbali kusafiri kwa haraka kuliko miaka ya
nyuma ambapo simu na barua kupitia sanduku la posta ndivyo vilivyokuwa njia kuu
za upelekaji taarifa. Kukua kwa teknolojia hizi za upashanaji habari ni matokeo
chanya ya kukua kwa ushindani katika sekta ya mawasiliano ulimwenguni.
Kukua kwa ushindani kumewezesha matumizi ya
teknolijia za kisasa katika uzalishaji pia, kumeibua njia rahisi za uzalishaji,
uuzaji na usambazaji wa bidhaa na huduma yakiwemo matumizi ya biashara mtandao.
Ndugu
Wanasemina
Mabadiliko haya ya sayansi, teknolojia na
utandawazi, mbali ya kuleta mafanikio yaliyoainishwa, pia yamesababisha
changamoto mbalimbali katika soko. Teknolojia imerahisisha kufanyika kwa
udanganyifu mkubwa katika soko unaosababishwa na wizi wa milikibunifu na alama
za bidhaa ulimwenguni kote. Tanzania pia imekabiliwa na changamoto za bidhaa
bandia zinazouzwa kiudanganyifu sokoni.
Ndugu
Wanasemina
Sera ya Biashara ya mwaka 2003, imebainisha
kuwa Tanzania imeamua kuanzisha mfumo wa kisasa wa usimamizi wa soko kwa kuweka
sheria za Ushindani na Udhibiti kwa madhumuni ya kudhibiti kasoro zilizopo
katika soko, hasa tabia ya ukiritimba wa soko (kuhodhi soko) ambayo huathiri na
kudumaza biashara katika uchumi wa soko.
Uchumi wa soko unahitaji washiriki wengi
kuweza kuingia na kufanya shughuli zao bila vikwazo na kuwepo kwa mazingira ya
fursa sawa kiushindani (level playing
field) ili faida zake ziweze kupatikana. Ni mfumo ambao unaongozwa na nguvu
ya uhitaji na ugavi (demand and supply).
Kwa lugha nyepesi kabisa, kama una wauzaji
bidhaa kama vipuri au vifaa vya umeme wachache sokoni, watakuwa wanahodhi soko
hilo na wanaweza wakala njama kuweka mikakati ya kumnyonya mlaji na kufifisha
ushindani baina yao. Mbinu na mikakati hiyo ni pamoja na kupanga bei, kugawana
masoko kijiografia, kuficha bidhaa, kutumia vibaya nguvu za soko na kuwaondoa
washindani sokoni.
Kukosekana kwa ushindani katika soko,
hudumaza tija, ubunifu na ukuaji wa viwanda kwa kusababisha vizuizi vya
washindani kuingia sokoni. Kwa upande mwingine, mlaji atakabiliwa na uhaba wa
bidhaa.
Ndugu
wanasemina
Baada ya Serikali kulegeza masharti ya
biashara, kumeibuka wimbi la wafanyabiashara wasio waaminifu kuingiza nchini
bidhaa zisizokidhi matarajio ya matumizi katika soko. Zipo bidhaa bandia, zipo
bidhaa duni na zipo bidhaa hatarishi kwa matumizi ya binadamu.
Tumesikia matukio ya ajali za moto kutokana
na vifaa vya umeme bandia. Tumesikia matukio ya wananchi kupoteza maisha baada
ya kutumia dawa na vipodozi hatarishi.
Aidha, ajali za vyombo mbalimbali vya moto zimehusishwa na matumizi ya
vipuri bandia katika vyombo hivyo.
Udhibiti wa soko unaofanywa na vyombo vyetu
vya kudhibiti bidhaa unalenga kuwakinga walaji dhidi ya vitendo potofu katika
biashara vinavyolenga kuwahadaa walaji. Hii itawawezesha wazalishaji wa bidhaa
halisi kupata soko la bidhaa zao na kuifanya Tanzania nchi inayovutia
wawekezaji.
Ndugu
Wanasemina
Tumewaita hapa leo ili tuweze kubadilishana
mawazo na kuelimishana masuala ya msingi yatakayotuwezesha kufanya biashara
zetu kwa njia ambazo ni endelevu na kwa wadhibiti na wasimamizi wa soko
kutekeleza majukumu yao kwa namna ambayo inazingatia uelimishaji na uwezeshaji.
Ndugu
Wanasemina
Ili kujenga mahusiano mazuri baina ya vyombo
vya Serikali vinavyohusika na udhibiti wa bidhaa na usimamizi wa soko,
wazalishaji na wafanyabiashara tunahitaji kufanya kazi kwa pamoja ili kuleta
ustawi wa biashara zetu na wananchi tunaowauzia bidhaa hizo.
Wadau wote wafahamu kwamba madhumuni ya
Serikali katika kusimamia uchumi wa soko si kukataza biashara bali kutaka
ifanyike kwa kuzingatia sheria na misingi ya ushindani. Hivyo, washindani
wanatakiwa kushindana na si kula njama za kukwepa kushindana sokoni.
Washindani watumie fursa iliyopo kutanzua
migogoro inayohusu ushindani baina yao kwa kutumia vyombo husika kama vile Tume
ya Ushindani na Baraza la Ushindani.
Aidha, Tume ya Ushindani pamoja na vyombo
vingine vya Udhibiti, vitekeleze majukumu yao kwa kuongeza zaidi utoaji wa
elimu kwa wafanyabiashara na kuwaelekeza zaidi kuhusu yawapasayo kutenda ili
kuepuka ukiukwaji wa sheria mara kwa mara.
Ndugu
wanasemina
Mwisho kabisa nivitake vyombo hivi vya
udhibiti na usimamizi wa soko kuongeza utendaji kazi kwa ushirikiano wa karibu,
kusisimaia kikamilifu
na kutoa huduma stahiki na kwa wakati. Tanzania si Jalala, na kamwe haiwezi kuwa
soko la bidhaa bandia kwa gharama ya uhai na maisha ya Watanzania.
Vile vile napenda kuwasisitiza
kuepuka rushwa na njama zozote za baadhi
ya wafanyabiashara walafi wanaopenda kutumia mbinu chafu ili kuua viwanda na biashara za wenzao ili wabaki peke yao, na hivyo kuwalazimisha
walaji kutumia bidhaa zao pekee. Mahali
pasipo na ushindani wa haki, hata viwango hushuka na bei huwa si za haki. (kiambatisho
Na (1) - hatua zilizochukuliwa 2016/17.
Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji haitasita kuchukua hatua stahiki kwa wote watakaojihusisha na mwenendo huo.
Ndugu
wanasemina,
Nafahamu kuwa Tume ya Ushindani wana
makubaliano rasmi na Shirika la Viwango kuendesha kaguzi za pamoja. Vile vile
Taasisi zote zinazohusika na masuala ya bandari zimeanza kufanya kazi kwa muda
wa saa ishirini na nne (24). Juhudi hizi kwa pamoja zitaifanya Tanzania kwa
kiwango kikubwa kuwa nchi ya kivutio cha uwekezaji kwa viwanda na sekta
nyingine mbalimbali. Hivyo, nawaomba
washiriki wa semina hii muwe wasikivu na wadadisi ili kuchangia ipasavyo ukuaji
wa uchumi wa viwanda katika nchi yetu.
Ndugu
wanasemina, Baada
ya kusema maneno haya machache, sasa natamka kuwa semina hii ya “umuhimu wa
sheria ya ushindani katika uchumi wa viwanda Tanzania” imefunguliwa rasmi.
Niwakumbushe
kauli Mbiu yetu "TANZANIA YA SASA
TUNAJENGA VIWANDA"
Mh. Mhandisi Stella M. Manyanya, (MB)
NAIBU
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
Tuesday, 5 December 2017
FCC Yaadhimisha Siku ya Ushindani Desemba 5, 2017
Dar es Salaam, Desemba 6, 2017. Tume ya Ushindani nchini Tanzania imeadhimisha Siku ya Ushindani Duniani kwa kutoa mafunzo kwa wadau wa vyombo vya udhibiti na wawakilishi wa vyama vya wafanyabiashara.
Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 5 Desemba, 2017 katika ukumbi wa GEPF, eneo la Victoria na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (MB), alikuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo.
Akifungua Rasmi maadhimisho hayo, Mhe. Naibu Waziri Manyanya aliwataka Wafanyabiashara kuepuka kuigeuza Tanzania jalala la bidhaa bandia. Aidha aliwaonya watendaji wa Serikali kuepukana na vishawishi vya rushwa katika kukagua bidhaa sokoni na katika maingilio ya bidhaa nchini.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dk. John Kedi Mduma alimweleza Naibu Waziri kuwa maadhimisho hayo yametokana na Makubaliano ya Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika tarehe 5 Desemba, 1980 ya kukubaliana kuhusu kanuni za kudhibiti vitendo vinavyodumaza ushindani duniani. Alibainisha kuwa nchi wanachama zinaadhimisha siku hii kuendelea kuwakumbusha watendaji katika mfumo wa biashara ulimwenguni kuzingatia misingi na kanuni za ushindani.
Mafunzo hayo yalihudhuriwa na watendaji kutoka Wakala wa Mbolea, Shirika la Viwango (TBS), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Chama cha Wenye Viwanda, Biashara na Kilimo (TCCIA), Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Anga (TCAA), Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na wadau wengine.
Wadau hao pia waliweza kuelezea uzoefu wao katika kushajiisha ushindani katika soko katika utekelezaji wa shughuli zao.
Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 5 Desemba, 2017 katika ukumbi wa GEPF, eneo la Victoria na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (MB), alikuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo.
Akifungua Rasmi maadhimisho hayo, Mhe. Naibu Waziri Manyanya aliwataka Wafanyabiashara kuepuka kuigeuza Tanzania jalala la bidhaa bandia. Aidha aliwaonya watendaji wa Serikali kuepukana na vishawishi vya rushwa katika kukagua bidhaa sokoni na katika maingilio ya bidhaa nchini.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dk. John Kedi Mduma alimweleza Naibu Waziri kuwa maadhimisho hayo yametokana na Makubaliano ya Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika tarehe 5 Desemba, 1980 ya kukubaliana kuhusu kanuni za kudhibiti vitendo vinavyodumaza ushindani duniani. Alibainisha kuwa nchi wanachama zinaadhimisha siku hii kuendelea kuwakumbusha watendaji katika mfumo wa biashara ulimwenguni kuzingatia misingi na kanuni za ushindani.
Mafunzo hayo yalihudhuriwa na watendaji kutoka Wakala wa Mbolea, Shirika la Viwango (TBS), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Chama cha Wenye Viwanda, Biashara na Kilimo (TCCIA), Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Anga (TCAA), Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na wadau wengine.
Wadau hao pia waliweza kuelezea uzoefu wao katika kushajiisha ushindani katika soko katika utekelezaji wa shughuli zao.
Sunday, 22 October 2017
Makala ya "Umuhimu wa Tume ya Ushindani Katika Uchumi Wetu" Kutoka Hotuba ya Prof. Adolf Mkenda Akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC, Dk. John Kedi Mduma na Kumshukuru Mkurugenzi Mkuu aliyemaliza Muda wake Dk. Frederick Ringo, mwishoni mwa Agosti, 2017
UMUHIMU WA TUME YA USHINDANI KATIKA UCHUMI WETU
Adolf F. Mkenda
[Makala hii
imeandikwa kutokana na dondoo za hotuba ya Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji
aliyoitoa kwa watumishi wa Tume ya Ushindani mwezi wa nane mwaka huu. Mwandishi
ndiye Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji kwenye Wizara ya Viwanda, Biashara
na Uwekezaji].
Leo
nimekuja kuzungumza na nyie kwa sababu kuu tatu. Sababu ya kwanza, nimekuja
kumtambulisha mtu ambaye Waziri amemteua kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa
Tume ya Ushindani, Dkt John Kedi Mduma. Utaratibu wa kumpata Mkurugenzi Mkuu
unaendelea kwa kuzingatia Sheria iliyounda Tume, kwa hiyo wakati utaratibu huu
unaendelea, Dkt Fredrick Ringo ambae muhula wake wa uongozi umeisha,
atamkabidhi Dkt Mduma majukumu ya kuongoza Tume. Mpeni Dkt Mduma ushirikiano
wote ili aweze kuendesha kazi hii vizuri katika kipindi hiki cha mpito.
Nimekuja
pia kumpa Dkt Fredrick Ringo ahsante kwa kazi aliyoifanya kuongoza Tume kwa
muhula aliotumikia kama Mkurugenzi Mkuu. Ahsante Dkt Ringo na tunakutakia
mafanikio katika majukumu yako mengine utakayoendelea nayo.
Sababu
ya tatu ya kutaka niwaone ni kuja kuwatia moyo na kuwahimiza muendelee na kazi
nzuri mnayofanya na kutumia fursa hii kunena mambo machache kuhusu Tume.
Kazi za Tume ni ngumu sana na zinagusa maslahi makubwa ya watu ambao mara nyingi wana uwezo mkubwa wa kifedha na ushawishi. Mkikamata bidhaa bandia na kuziteketeza mnawatia hasara wale waliotengeneza au kuingiza bidhaa hizo hapa nchini; wanapoteza mamilioni na mabilioni ya fedha. Watu hawa hawatafurahi na watafanya kila njia kupambana na nyie, ikiwa ni pamoja na kuwapikia majungu. Mkiingilia mikakati ya makampuni ambayo yanataka kutumia hila ili yahodhi soko na kuumiza walaji na watu wadogo wanaozalisha malighafi mnaharibu ndoto za utajiri za makampuni haya. Hila za kujenga umiliki wa kuhodhi soko, yaani monopoly power, zinafanywa na watu ambao wana nguvu za kiuchumi na hata kisiasa kwa hiyo kupambana nao ni lazima kujifunga kibwebwe kweli kweli.
Lengo
lenu jema na la kisheria la kuthibiti nyendo zisizo za ushindani wa haki
linawalemea wale ambao wangependa uchumi wetu uendeshwe kwa ubabe wa mwenye
nguvu mpishe, kwa kutumua the law of the
jungle. Wababe hawa siku zote
watapambana na nyie kwa kila namna watakavyoweza.
Napenda
kuwahakikishia kwamba Serikali iko pamoja na nyie na itasimama kidete
kuhakikisha mnatekeleza majukumu yenu kwa mujibu wa sheria bila kutetereka.
Chapeni kazi! Tutawalinda na kuwatetea kwa kazi mnazozifanya mradi tu mnafuata
sheria, weledi na uadilifu.
Nawahakikishia pia kwamba tunajua sheria ni msemeno, na sheria haijali mkubwa wala mdogo, inajali tu haki. Serikali haitawaingilieni katika kutekeleza majukumu yenu kwa mujibu wa sheria na msikubali kuingiliwa na mtu yeyote. Tukianza kuwaingilia katika utendaji wenu, tutaharibu kabisa dhana nzima ya uchumi huria unaoongozwa kwa sheria na kanuni. Tukienda huko tutaacha kujenga uchumi ambao ni rule based na kujenga uchumi wa deal making. Lakini nyote mmemsikia Rais wetu akisisitiza vita dhidi ya rushwa, dhidi ya wapiga dili. Hatutakubali kujenga uchumi wa wapiga dili, tunajenga uchumi huria unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria na kanuni.
Na
ni vyema mkajua kwamba zama hizi, kuliko zama zilizopita, jukumu la mamlaka za
usimamizi na udhibiti ni kubwa na muhimu zaidi. Kwanza, ni kwa sababu tumeamua
kujenga uchumi wa soko huria. Kwa kujenga uchumi wa soko huria tunaachia uhuru
wa watu kuzalisha na kuuza bidhaa zao bila kupangiwa na Serikali au mamlaka
nyingine yeyote. Uhuru ni haki ya binadamu, kwa hiyo ujenzi wa soko huria ni
hatua nyingine ya kupanua uhuru wa binadamu. Haki hii haihitaji sababu nyingine
yeyote kuitetea, kwani, kama alivyosema Mwalimu Nyerere kupitia Mwongozo wa
TANU wa Mwaka 1971, kwa wanadamu, “ kitendo chochote kinachowapa uwezo zaidi wa
kuamua mambo yao wenyewe, ni kitendo cha maendeleo, japo kama hakiwaongezei
afya wala shibe”. Kwa bahati nzuri, hatua ya kuongeza uhuru wa kiuchumi ni
hatua ambayo kwa kawaida huongeza pia tija na ufanisi, na hivyo kukuza zaidi
uchumi kwa ujumla. Kwa hiyo tuna sababu nzuri ya ziada ya kujenga na kuimarisha
uchumi wa soko huria.
Lakini
ujenzi wa soko huria sio kuachia mambo kiholela. Ni lazima bidhaa
zinazozalishwa ziwe salama na zikidhi viwango. Mzalishaji na muuzaji wanao
uhuru, lakini sio uhuru wa kumdanganya mlaji na kuuza bidhaa zenye madhara au
ambazo hazina viwango vinavyotarajiwa na mlaji. Kadhalika, soko huria halina
maana mzalishaji mmoja afanye hila kuwamaliza wazalishaji wengine ili ahodhi
soko mwenyewe. Yeyote anayefanya hila za namna hii nia yake ni kuwapunja wale
wanaomuuzia mali ghafi, kwa sababu mnunuzi atakuwa mmoja tu au watakuwa
wachache ambao wanaweza kuunganisha mikakati yao, na pia nia inakuwa ni
kuwaumiza walaji, kwani ukiondoa ushindani inakuwa rahisi kupandisha bei ya
bidhaa ili kupata faida kubwa kupita kawaida. Soko huria haliruhusu uzalishaji
wa hila, kwa kuingilia haki-miliki za wengine na kuzalisha bidha bandia, jambo
ambalo linadhoofisha ubunifu na lina tabia ya kuzalisha bidhaa zisizokidhi
viwango vya ubora na usalama. Soko huria linaendeshwa kwa kanuni, kanuni zinazo
lenga kulinda haki ya walaji na wazalishaji, kuongeza ubunifu na kukuza
ushindani wa haki usio na hila na ghiliba.
Kwa sababu sasa tumeingia katika ujenzi wa uchumi huria, kazi za mamlaka za usimamizi na udhibiti zimezidi kuwa muhimu ili kutuepusha na ujenzi wa uchumi holela. Kama nilivyosema, tunataka kujenga uchumi huria unaofuata kanuni, yaani rule-based economy, badala ya kujenga uchumi holela unaotegemea tu nani anamjua nani. Hatutaki uchumi wa deal-making, uchumi wa mwenye nguvu mpishe.
Ipo
sababu kubwa ya ziada inayofanya shughuli za mamlaka za udhibiti na usimamizi,
kama Tume ya Ushindani, kuwa muhimu zaidi katika zama hizi. Hii ni kwa sababu
Serikali, kupitia Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, imeamua kutenga miaka
hii mitano mahsusi kwa ajili ya ujenzi wa uchumi wa viwanda. Tume ya Ushindani
na mamlaka nyingine za udhibiti na usimamizi kama TBS na TFDA ni muhimu sana
katika kuchochea ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa sababu zinasimamia ubora na
usalama na kujenga mazingira ya ushindani wa haki, mambo ambayo ni muhimu sana
kwa wazalishaji na walaji.
Kama
bidhaa za viwandani zinazozalishwa nchini hazitakidhi viwango vya ubora na
usalama, wananchi wataendelea kupendelea bidhaa zinazoagizwa kutoka nje ya
nchi, na hivyo kudhoofisha uzalishaji wa ndani. Lazima tukumbuke kwamba kwa
kuwa wanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo ya
Kusini mwa Afrika takribani nchi ishirini na mbili zina haki ya kuingiza bidhaa
zake nchini mwetu bila ukomo na bila ushuru wa forodha. Kwa hiyo hatuwezi
kutegemea ushuru wa forodha kulinda bidhaa za ndani dhidi ya ushindani kutoka
EAC na SADC; hatuna budi kujifunga kibwebwe na kendelea kuongeza ubora wa
bidhaa zetu. Hiyo ndiyo salama yetu.
Lakini
pia uzalishaji wa ndani unahitaji kutumia masoko ya nje. Jitihada za ujenzi wa
uchumi wa viwanda miaka ya sitini na sabini zilishindwa kwa sababu zilijikita
zaidi katika kuzalisha bidhaa kukidhi matakwa ya ndani, bila kujali sana
umuhimu wa kuzingatia ushingani kwenye masoko ya nje, kwa kile kilichoitwa Import Substitution Industrial Strategy.
Jitihada hizi zilitegemea sana matumizi ya ushuru wa forodha na uthibiti wa
fedha za kigeni kulinda viwanda vya ndani. Mkakati huu ulishindwa kwa sababu
kadhaa, na sasa hivi mkakati kama huu utashindwa zaidi kwa sababu ya kasi ya
utandawazi. Ukweli ni kwamba utandawazi ni wimbi ambalo ukipigana nalo kama
mkakati wa kudumu unazama, ukiogelea utaelea na unaweza kufanikiwa sana. Hapa
maneno ya gwiji Shakespeare yana maana kubwa sana, kwamba:
Na
zaidi ya hapo, ni lazima sasa kuliko wakati wote tuzuie kabisa uingizwaji wa
bidhaa zisizo na viwango na bidhaa bandia kutoka nje ya nchi. Hapa Tume
inajukumu kubwa sana. Bidhaa hizi zisizo na viwango na zile bandia zinapoingia
nchini zinadhoofisha sana uzalishaji wa ndani kwa kuleta ushindani usio wa haki
na kudhulumu walaji.
Lazima
tukubali kwamba bidhaa bora, salama na zisizo bandia kutoka nje zitaendelea
kuingia nchini. Baadhi ya bidhaa hizo zitatoka nchi za Jumuiya ya Afrika ya
Mashariki na nchi za SADC, na hivyo zitaingia nchini bila kutozwa ushuru wa
forodha na bila kuwekewa ukomo. Bidhaa hizi zitaleta ushindani mkubwa kwa
wazalishaji wa ndani. Lazima tukubali kuwa ushindani wa haki ni jambo jema.
Ushindani wa haki humnufaisha mlaji kwa kumpa bidhaa bora na salama kwa bei
ahueni. Ushindani pia hulazimisha wazalishaji wengine kuacha kubweteka na
badala yake kuongeza ubunifu na ubora wa bidhaa zao. Kwa maana hiyo ushindani
ni jambo bora sana. Maana ya hoja hii ni kwamba uzalishaji wa ndani hauna budi
kukidhi viwango vya kimataifa, na mamlaka zetu za udhibiti na usimamizi zina
kazi ya kufanikisha jambo hili. Hii ni kazi kubwa, lakini ni kazi ya lazima ili
tuweze kuhimili ushindani ndani na kukabiliana na ushindani kwenye masoko ya
nje.
Tume
ya Ushindani, kwa kuondoa hila na ghiliba katika masuala ya uchumi wetu, inasaidia
sana kujenga mazingira mazuri ya ushindani, mazingira ambayo yanaongeza ubunifu
ambao unapunguza gharama za uzalishaji na kuongeza usalama na ubora wa bidhaa
zinazozalishwa nchini. Dhima yenu hii adhimu haionekani moja kwa moja, lakini
kwa hakika kazi yenu inasaidia wazalishaji wetu wasibweteke na wajue kwamba
hakuna njia za panya za ghiliba. Na hii inasaidia sana kufanya wazalishaji wetu
wawe washindani.
Kazi
ya Tume ina mwelekeo wa kimahakama, na mahakama haiwezi kufanya kazi zake kwa
haki bila kuwa huru. Kama nilivyosema, Serikali haitawaingilia katika majukumu
yenu, badala yake itawalinda na kuwatetea mnapotekeleza majukumu yenu kwa
mujibu wa sheria.
Walakini
ningependa kuongeza mambo machache. Kuwa huru na kufuata sheria kusiwafanye
mtekeleze majukumu yenu kibabe. Kazi yenu ni kusimamia sheria pasipo
kutetereka, lakini kufanya hivyo kwa weledi na uadilifu. Kazi yenu sio kukomoa,
kazi yenu ni kufanikisha na kuwezesha.
There is a tide
in the affairs of men.
Which, taken at
the flood, leads on to fortune;
Omitted, all the
voyage of their life
Is bound in
shallows and in miseries.
Utandawazi
umetushika, na ukishikwa shikamana. Ni muhimu tuchukulie utandawazi kama fursa
ya sisi kuzalisha na kuuza kwenye masoko ya nje. Ujenzi wa uchumi wa viwanda
ambao unalenga siyo tu kukidhi mahitaji ya ndani bali pia kuzalisha na kuuza
kwenye masoko ya nchi za nje una faida kubwa nyingi. Kwanza unavutia wawekezaji
wenye mitaji mikubwa, ambao wanajua kwamba ili kupunguza gharama za uzalishaji
ni muhimu kizalisha kwa wingi mkubwa, wingi ambao soko la ndani peke yake
linaweza lisimudu kununua bidhaa zote. Kwa kupunguza gharama za uzalishaji
kupitia kwa wingi wa uzalishaji viwanda vyetu vitaweza kuwauzia walaji wa ndani
bidhaa kwa bei ahueni na wakati huo huo kuweza kushindana kwenye soko la dunia.
Zaidi ya hapo, kupanua uzalishaji wa viwanda kukidhi mahitaji ya ndani na
kufukuzia masoko ya nje kutahakikisha kwamba ajira inazalishwa kwa wingi hapa
nchini.
Hapana
shaka kabisa kwamba ili kuweza kuuza bidhaa zetu kwenye soko la dunia, suala la
usalama na ubora ni lazima yazingatiwe kwa kiwango cha juu. Kadhalika
wazalishaji wa ndani wanaotegemea zaidi hila za kuhodhi soko la ndani kwa kudhoofisha
ushindani, hawataweza kumudu ushindani kwenye soko la dunia. Kwa hiyo kazi za Tume
na mamlaka nyingine za udhibiti na usimamizi ni muhimu sana katika kutuweka
sawa kushindana kwenye masoko ya nje.
Serikali
imeongeza nguvu katika kuboresha mazingira ya kufanya shughuli za kiuchumi
nchini mwetu, na moja ya maeneo ambayo yamemulikwa sana ni kile kinachoitwa
utitiri wa tozo, ada na masharti ya mamlaka mbali mbali za usimamizi na udhibiti.
Kazi kubwa tayari imeshafanyika na mapendekezo yameandaliwa ya kuboresha
mazingira ya kufanya shughuli za kiuchumi nchini. Zoezi hili ni endelevu, hivyo
Tume, kama ilivyo kwa mamlaka nyingine, mna wajibu wa kupitia mapendekezo
ambayo karibuni yatachapishwa kwa minajili ya kuona ni wapi Tume ifanye
maboresho. Katika utendaji wetu wa kila siku ni budi kujitahidi kuvumbua hatua
za ziada ambazo kama zitachukuliwa zitasaidia kufanya mazingira ya biashara na
uchumi kuwa bora zaidi. Kwa hiyo Tume sasa inabidi, pamoja na kutekeleza
majukumu yake ya kisheria, ijikite pia katika kusukuma mageuzi ya kuboresha
mazingira ya biashara na uchumi, na tufanye jambo hili kama moja ya majukumu
yetu.
Hata
hivyo, kadiri mnavyoongeza kasi ya kutekeleza majukumu yenu ndivyo pia
manung’uniko yatakavyo ongezeka. Hilo mlitegemee. Kwa kiasi kikubwa Tume
itaonwa kama kero na suala hili litafikishwa kwenye medani za kisiasa mara
nyingi tu. Ili mradi mnafanya kazi zenu kwa weledi na uadilifu, jambo hili
halipaswi kuwatisha wala kuwakatisha tamaa.
Badala yake ongezeni nguvu katika kuuelimisha umma kuhusu umuhimu wa
majukumu yenu. Tumieni kila fursa inayowezekana kuelimisha umma ili watu
waelewe na kukubali majukumu yenu muhimu.
Lakini
ni vyema mkajua kuwa kikipatikana kisa kimoja tu cha mtumishi wa Tume
atakayekiuka maadili na weledi wa kazi yake, kisa hiki ndicho kitakachotumika
na wote wenye manung’uniko kuharibu kabisa taswira ya Tume. Kisa kimoja tu
kinatosha kuharibu sana kazi yenu nzuri. Kwa hakika msemo wa samaki mmoja
akioza tenga lote limeoza ni muhimu sana kwa Tume katika zama hizi. Msikubali
kabisa yeyote miongoni mwenu aharibu taswira ya taasisi hii muhimu. Endapo
kutatokea kisa cha ukosefu wa weledi na uadilifu, chukueni hatua kali haraka
sana kwa mujibu wa sheria na taratibu za utumishi. Katika hili pia Serikali
itakuwa na nyie bega kwa bega. Ahsanteni.
LIMETOLEWA NA TUME YA USHINDANI (FCC)
Wednesday, 20 September 2017
FCC Katika Channel Ten Alhamisi Septemba 21, 2017
Usikose mahojiano maalum katika Channel Ten tarehe 21 Septemba, 2017 kuanzia saa nne kamili hadi nne na nusu usiku. Maimu Mkurugenzi Mkuu, Dk. John Kedi Mduma, Kaimu Mkurugenzi wa Utetezi wa Mlaji na Udhibiti wa Bidhaa Bandia, Godfrey Gabriel, Mkuu wa Idara ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia, Zaytun Kikula na Afisa Mkaguzi wa Bidhaa Bandia, Mike kajembe, watashiriki katika mahojiano yatakayooendeshwa na Mtangazaji Donald Mtani.
USIKOSE.
Wednesday, 6 September 2017
Picha za Vikao vya Kurugenzi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC
Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji, Bibi Anne Mbughuni, akimweleza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume, Dk. John Kedi Mduma (kushoto), kuhusu shughuli za kurugenzi yakı katika ukumbi wa mikutano wa Tume, Septemba 5, 2017.
Wafanyakazi wa Kurugenzi ya Uendeshaji wakifuatilia wasilisho la Kaimu Mkurugenzi wao, Bibi Anna Mbughuni katika kikao na Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Dk. John Kedi Mduma katika ukumbi wa mikutano wa Tume, Septemba 5, 2017.
Wafanyakazi wa Kurugenzi ya Uendeshaji wakifuatilia wasilisho la Kaimu Mkurugenzi wao, Bibi Anna Mbughuni katika kikao na Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Dk. John Kedi Mduma katika ukumbi wa mikutano wa Tume, Septemba 5, 2017.
Wafanyakazi wa Kurugenzi ya Utetezi wa Mlaji na Udhibiti wa Bidhaa Bandia wakifuatilia wasilisho la Kaimu Mkurugenzi wao, Bw. Godfrey Gabriel katika kikao na Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Dk. John Kedi Mduma katika ukumbi wa mikutano wa Tume, Septemba 5, 2017.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC, Akutana na Wafanyakazi
Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC Akutana na Kuzungumza na Wafanyakazi
DAR ES SALAAM, Septemba
5, 2017. Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dk. John Kedi Mduma, amefanya
mikutano na Kurugenzi zote za Tume ya Ushindani ili kujifunza kuhusu shughuli
za Kurugenzi hizo na idara zilizo chini ya Kurugenzi hizo na kujua shughuli wanazozifanya, mafanikio na changamo wanazokabiliana mazo.
Kurugenzi zilizohusika na vikao hivyo ni pamoja na Kurugenzi
ya Miungano ya Kampuni, Utafiti na Utetezi wa Ushindani, inayoongozwa na Dk.
Allan S. Mlulla, Kurugenzi ya Kushughulikia Makosa Yanayodhiisha Ushindani,
inayoongozwa na Dk. Deo Nangela, Kurugenzi ya Utetezi wa Mlaji na Udhibiti wa
Bidhaa Bandia inayoongozwa na Godfrey Gabriel.
Kurugenzi hizo zilielezea shughuli zake zilizopo katika mpango
kazi, vipaumbele, changamoto na namna wanavyokabiliana nazo.
Katika mikutano hiyo, majadiliano ya namna ya kuboresha
utendaji pia yalifanyika.
Kaimu Mkurugenzi huyo alitambulishwa kwa wafanyakazi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Vianda, Biashara na Uwekezaji (anayeshughulikia biashara na uwekezaji), Profesa Adolph Mkenda, siku alipoanza kazi rasmi kushika wadhifa huo, tarehe 28 Agosti, 2017.
Monday, 4 September 2017
Toa Taarifa Unapokutana na mikataba inayomkandamiza mlaji
Wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakiweka mikataba inayokwepa uwajibikaji na kumkandamiza mlaji. Kuanzia Januari 1, 2016, Tume imeanza kupokea, kupitia na kusajili mikataba ya mlaji inayoandaliwa na mto huduma kwa nia ya kuonda vipengele vinavyokwepa uwajibikaji na kumkandamiza mlaji. Unapokuwa katika shughuli za kupata huduma ukakutana na mikataba ya huduma kwa mlaji ya aina hii, wasiliana na Tume ya Ushindani kwa Namba ya simu 22 2926128-31. Barua pepe info@competition.or.tz
Thursday, 31 August 2017
Picha za Baadhi ya BIdhaa Bandia zilizokamatwa
Kijiko (Fork Lift) chenye alama ya kughushi ya HELI.
Vijiko (Fork Lifts) zenye alama ya kughushi ya HELI zikiondoshwa eneo zilipokamatwa.
Sampuli za viatu vilivyokamatwa kwa kughushi nembo zisizo mali yao.
Spika zilizokamatwa kwa kughushi nembo.
Moja ya Spika zilizokamatwa kwa kughushi nembo.
Sampuli ya viatu vilivyokamatwa kwa kughushi nembo isiyo mali yao.
Wakaguzi wa Tume wakipata mafunzo ya namna ya kutambua kofia ngumu za usalama kwa waendesha pikipiki zilizoghushiwa alama ya FEKON.
Sehemu ya shehena ya kofia ngumu za usalama kwa waendesha pikipiki aina ya FEKON zilizokamatwa.
Sehemu ya shehena ya viatu bandiavilivyokamatwa.
Sehemu ya shehena ya viatu bandiavilivyokamatwa.
FCC Seize Counterfeit Goods Worth TZS 441,355,530/-
PRESS RELEASE
FCC Seize Counterfeit Goods Worth
TZS 441,355,530/-
DAR ES SALAAM, 30th
August, 2017. The
Fair Competition Commission (FCC), acting pursuant to the Merchandise Marks
Act, No. 8 of 2003, has conducted a Search and Seizure operation in Dar es
Salaam and Mtwara between January and July, 2017 and seized various counterfeit
goods worth TZS 441,355,530/- the goods include
1. 59 pieces of counterfeit FIDEK
Musical Speakers valued at TZS 53,100,000/-,
2. 30 pieces of counterfeit crown
musical speakers valued at TZS 15,000,000/-
3.
1,246 pieces of counterfeit FEKON Motorcycle helmets valued at
TZS
4.
18,640,000/=
5.
Eight (8) counterfeit SANLG Motorcycles and seven (7) counterfeit motorcycle engines valued at TZS 19,400,000/-
6. Three units of Counterfeit HELI FORK
LIFTS valued at TZS 167,607,765/-
7. 5889 pairs of counterfeit PUMA
Footwear (shoes) valued at TZS 235,560,000
All search and seizure operations were prompted by market
surveillance and investigation reports made by FCC.
Businessmen whose goods were seized
during the said operations are at various stages of complying with the
penalties issued to them in line with the Merchandise Marks Act (963), as
amended and the MMA Regulations.
The FCC warns wholesale and retail
sale businessmen and women to desist from engaging in counterfeit goods as the
same is a criminal offence and is punishable by fines and jail terms.
Counterfeit goods also create
uneven playing field and scares away investors from setting up production
plants in the country.
Consumers are equally advised to
check products for wholesomeness before committing their money in buying them.
They are also advised to check for product information including manufacturer’s
addresses ,country of origin, user manuals and warranty certificates and to
demand a legitimate receipt for all their purchases. They have an obligation of
reporting any conduct that infringe their rights at the market to relevant
authorities, including the FCC.
FCC offices are located on the
second floor of the GEPF House, Regent Estate, Bagamoyo Road. Aggrieved consumers
can also call +255 22 2926128/29/30.
Search and Seizure operations as
well as entry point inspections for counterfeit goods are continuous
undertakings and businesses should voluntarily comply with the law.
For Further clarifications please
consult Mr. Frank S. Mdimi, Senior Communications and Public Relations Officer,
Fair Competition Commission, Mobile +255-784762437, E-mail: fmdimi@competition.or.tz
FCC Yakamata Bidhaa Bandia za Thamani ya TZS 441,355,530/-
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
FCC Yakamata Bidhaa Bandia za Thamani ya
TZS 441,355,530/-
DAR ES SALAAM, Agosti
30, 2017. Tume ya
Ushindani, ikifanya kazi kwa mujibu wa Sheria ya Alama za Bidhaa ya mwaka 1963,
iliyorekebishwa, imefanya kaguzi za kushitukiza katika maeneo mbalimbali ya
Jiji la Dar es Salaam na Manispaa ya Mtwara na kukamata bidhaa bandia zenye
thamani ya TZS 441,355,530/- kati ya Januari na Julai, 2017. Bidhaa
zilizokamatwa ni pamoja na:
1. Spika 59 za muziki zilizokuwa na
nembo ya kughushi ya FIDEK, zenye thamani ya TZS TZS 53,100,000/-,
2. Spika 30 za muziki zilizokuwa na
nembo ya kughushi ya Crown, zenye thamani ya TZS 15,000,000/-,
3.
Kofia ngumu za waendesha pikipiki 1,246 zilizokuwa na nembo ya kughushi ya FEKON zinazokadiriwa kuwa na thaman
ya TZS 18,640,000/=
4.
Pikipiki nane (8) zilizokuwa na nembo ya kughushi ya SANLG pamoja na injini 7
za pikipiki, vyote vikiwa na thamani ya TZS 19,400,000/-
5. Vijiko vitatu vya kubebea mizigo
vilivyokuwa na nembo ya kughushi ya HELI na vyenye thamani ya TZS 167,607,765/-
6. Jozi 5,889 za viatu zilizokuwa na
nembo ya kughushi ya PUMA, zenye thamani ya TZS 235,560,000/-.
Mazoezi yote ya kaguzi za
kushitukiza yaliyotokana na taarifa za ukaguzi wa masoko na uchunguzi wa bidhaa
bandia katka soko.
Wafanyabiashara waliokamatwa na
bidhaa hizo bandia wapo katika hatua mbalimbali za kukamilisha matakwa ya
sheria kuhusiana na adhabu walizopewa baada ya kukutwa na bidhaa hizo, kama
ilivyoainishw akatika Sheria ya Alama za Bidhaa (183), iliyorekebishwa pamoja
na kanuni zake.
FCC inawaasa wauzaji jumla na
rejareja wa bidhaa zote kujiepusha na biashara ya bidhaa bandia kwa kuwa
kufanya hivyo ni kosa la jinai linaoadhibiwa kwa faini na vifungo hela.
BIashara ya bidhaa bandia
husababisha ushindani usio haki sokoni kwa na unawakimbiza na kuwaogopesa
wawekezaji wa viwanda kuanzisha shughuli zao hapa nchini.
Walaji pia wanaaswa kukagua bidhaa
wanazozinunua sokoni kabla ya kuzilipia. Wanatakiwa kugaua ukamilifu wa bidhaa,
maelezo ya bidhaa ikiwa ni pamoja
na anuani ya mtengenezaji, nchi ya uasili, maelezo ya matumizi, vyeti vya
uthibitiho wa ubora wa bidhaa kutoka kwa mtengenezaji. Aidha, walaji wana
wajibu wa kudai risiti stahiki kw akila manunuzi waliyoyafanya. Pia wanatakiwa
kutoa taarifa za matukio ya ukiukwaji wa haki na maslahi yao katika Tume na
vyombo vingine.
Ofisi za FCC zipo Ghorofa ya pili
ya jengo la GEPF, Barabara ya Bagamoyo, simu namba +255 22 2926128/29/30.
Kaguzi za kushitukiza katika maeneo
binafsi ya kibiashara pamoja na kaguzi za kila siku katika maeneo ambayo ni
maingilio ya bidhaa (bandarini na bandari kavu) ni mazoezi endelevu,
Wafanyabiashara wote wanatakiwa kutii matakwa ya sheria ya alama za bidhaa bila
shuruti.
Kwa maelezo zaidi wasiliana
na Frank S. Mdimi, Afisa Mwandamizi, Mawasiliano na Mahusiano ya Umma, Tume ya
Ushindani, Simu ya Kiganjani +255-784762437, Barua Pepe: fmdimi@competition.or.tz
Tuesday, 29 August 2017
Dr. John Kedi Mduma Appointed New Acting DG of FCC
PRESS STATEMENT
Prof. Mkenda Introduces Dr. John
Mduma as the Acting Director General of FCC
Urges
Staff to Continue Working Diligently and Observe Integrity
Dar
es Salaam, 29th August, 2017. The Permanent Secretary at the
Ministry of Industry, Trade and Investments (Responsible for Trade)), Prof. Prof.
Adolph Mkenda, has urged FCC staff to continue working more diligently and
observe a high level of integrity as he spoke to them at their office premises
located in the GEPF House along Bagamoyo Road, on 28th August, 2017.
Prof. Mkenda gave such utterance as he was introducing to FCC staff the newly
appointed Acting Director General of FCC, Dr. John Kedi Mduma, a Senior
Lecturer and Economist from the University of Dar es Salaam who will take over
duties and responsibilities from Dr. Frederick Shadrack Ringo (Advocate), whose
tenure as the institution’s Director General ended on 1st August,
2017.
Speaking at the meeting, Prof. Mkenda pointed out that
he is aware of the immense importance and challenging duties and
responsibilities the Commission faces as a Market Support Institution and
called on staff to observe professionalism and integrity in order to safeguard
and project a correct institution’s reputations and corporate image which has
been carried well so far by the diligent performance of the Commission in
discharging its duties. He added that the same would positively contribute to
the Government’s vision of having in place an industrialised economy in line
with the requirements of the vision 2025, which seek to have the country move
to a middle income economy.
Prof. said that the Government would never tolerate
unequal playing field scenario created by unscrupulous traders importing and
selling into the country counterfeit goods. He said such acts should be
severely punished as they demoralise the efforts of genuine traders and scare
away investors from establishing industries in the country. He said that under
unequal playing field of that nature, investors shy away to set up industries
in Tanzania as they would not be able to compete with cheap counterfeits, which
also happen to be below the quality.
“The Government fully supports you, we shall keep on
protecting you, Go and work even more diligently, do not fear or favour anybody
and don’t be disheartened. Stand by the law all the time. However, You are now
required to apply even more professionalism and exercise a high level of
integrity to preserve the institutional image”, stressed Prof.
Mkenda. He called on all management and staff to accord the newly appointed
Acting Director general, Dr. John Mduma, requisite cooperation and assistance
with a view to realising higher institutional milestones in enforcing the legal
mandate entrusted to the Commission.
Prof. Mkenda commended the FCC staff for the good job
they are doing in regulating the market with high integrity amid scarce human,
fiscal and operational resources and promised to that the Government is aware
and will work towards uplifting their welfare as the condition may permit.
“However, as the workload and the welfare are set to
increase, and that the relevance of your responsibility as a market support
institution is going to be given a higher impetus, we shall always monitor your
performance to ensure that none of you will cause the Government’s efforts to
fail. Therefore, while continuing to do the good job, guard yourselves against
tarnishing the good image of your institution,” Prof. Mkenda
Stressed.
“The Government will not interfere with your
“Quasi-Judicial Powers” and decisions emanating from the same. We will however
ask for clarifications in order to know the truth, as and when needs arise.
Please do bear with us on that. Your job is difficult and as such, unfaithful traders
will seek to level false accusations against you in order to protect their
interests. We may be compelled to ask for clarifications from time to time. The
best shied against such people will be to observe a high level of integrity and
working even more diligently and protect the institutional corporate image
zealously as one protects his/her eyeball,” urged Prof.
Mkenda. He also pointed out that the Government would also not tolerate monopolistic
tendencies, which tend to suppress consumer choice and kill competition in the
market. . He urged Commission staff to continue taking requisite measures to
protect the market against such tendencies but should work in a more
facilitative manner. He specifically pointed out that the Commission should provide
pre-shipment advisory services to businessmen to help them avoid falling prey
to international counterfeit rings every now and then.
Prior to introducing Dr. Mduma to FCC staff, Prof.
Mkenda commended Dr. Frederick Shadrack Ringo for leading the institution
successfully and professionally in his four years tenure. He bid him farewell
and every success after the end of his tenure.
In the same vein, Dk. Frederick Ringo expressed his
sincere appreciation to the Government and staff of FCC for extending to him
the much needed cooperation and assistance which moved the institution a step
higher compared to where it was during his entrance. He also pointed out that
FCC has a shortage of more than 50 staff and would work even better if it would
have its own office premises and warehouses for storing seized counterfeit
goods awaiting destruction upon completion of legal proceedings.
Speaking after being introduced to FCC Staff, Dr. John
Mduma expressed his appreciation for the warm welcome and promised to point out
his priorities while speaking to staff after official assumption of the duties
in a short while to come.
Dr. John Kedi Mduma, an Economist and a Senior
Lecturer at the University of Dar es Salaam, was appointed by the Minister of
Industry, Trade and investments, Hon. Charles Mwijage (MP) to head the FCC
during the transition period from 28th August, 2017 while efforts to
have in place a substantive CEO are being worked out in line with the Fair
Competition Act No. 8 of 2003.
Issued
by the Communications and Public Relations Unit, Fair Competition Commission, Dar
es Salaam.
For
additional information please consult Frank S. Mdimi. Senior Communications and
Public Relations Officer, Fair Competition Commission, Calls/Whatsapp/SMS through
Mobile No. +255784762437, E-mail fmdimi@competition.or.tz
Subscribe to:
Posts (Atom)