Friday 18 May 2018

FCC Yawafanyia Semina Wafanyabiashara wa Pikipiki na Spea Zake

Tume ya Ushindani (FCC) imefanya semina wezeshi kwa wafanyabiashara wa pikipiki na spea zake jijini Dar es Salaam Februari 26, 2018.
 
Semina hiyo iliyohudhuriwa na wawakilishi takriban 30 wakiwemo viongozi wa Chama cha Wafanyabiashara hao, CHAWASAPI, pamoja na wafanyabiashara wa pikipiki na spea zake, ilifunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji Uwekezaji katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Leo Lyayuka.
 
Akifungua semina hiyo alibainisha kuwa jukumu la FCC ni sawa na mwamuzi wa kati katika mpira wa miguu na chombo hicho kimeamua kuwapatia elimu ili kuongezea nguvu eneo la utekelezaji sharia.
 
Mada mbalimbali ziliwasilishwa katika semina hiyo na wafanyabiashara hao kwa ujumla waliishukuru na kuipongeza FCC kwa kuendesha semina hiyo wezeshi. Aidha, waliishauri Tume kuongeza upelekaji wa semina za aina hiyo kwa wafanyabiashara waliopo mikoani ili kuwawezesha wafanyabiashara kuwa wadau muhimu katika ukuaji wa uchumi.
 
 

No comments:

Post a Comment