Friday 18 May 2018

Picha za Semina ya FCC na CHAWASAPI

Mwenyekiti wa CHAWASAPI, Bw. Martin Mbwana (kulia) akipeana mkono na Mgeni Rasmi, Bw. Leo Lyayuka, Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji Uwekezaji katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, baada ya hotuba ya ufunguzi ya mgeni rasmi, katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Utetezi wa Mlaji na Udhibiti wa Bidhaa Bandia, Bi. Magdalena Utouh. 

 Washiriki wa Semina ya FCC na CHAWASAPI iliyofanyiak katika ofisi za Tume Februari 26, 2018 wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Bw. Leo Lyayuka, Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji Uwekezaji katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji baada ya ufunguzi wa semina hiyo.

 Mgeni Rasmi katika semina ya CHAWASAPI, Bw. Leo Lyayuka, Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji Uwekezaji katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, akizungumza na Kaimu Mkurugenzi wa Utetezi wa Mlaji na Udhibiti wa Bidhaa Bandia, Bi. Magdalena Utouh (kushoto) na Msemaji wa CHAWASAPI, Bw. Award Mpandila (kulia) baada ya ufunguzi wa semina hiyo iliyofanyika katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018.

  Mwenyekiti wa CHAWASAPI, Bw. Martin Mbwana akizungumza na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa Semina ya FCC na CHAWASAPI iliyofanyika katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018.
 
   Mkuu wa Idara ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia, Zaytun Kikula, akiwasilisha mada kuhusu udhibiti wa bidhaa bandia wakati wa Semina ya FCC na CHAWASAPI iliyofanyika katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018.

    Afisa Mkaguzi wa Bidhaa Bandia na Utetezi wa Mlaji, Diana Augustine, akiwasilisha mada kuhusu Mahitaji na Matakwa, wakati wa Semina ya FCC na CHAWASAPI iliyofanyika katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018.

   Mwenyekiti wa CHAWASAPI, Martin Mbwana, akizungumza  wakati wa Semina ya FCC na CHAWASAPI iliyofanyika katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018.

    Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Dk. John K. Mduma, akizungumza wakati wa Semina ya FCC na CHAWASAPI iliyofanyika katika ofisi za Tume, Februari 26, 2018.

FCC Yawafanyia Semina Wafanyabiashara wa Pikipiki na Spea Zake

Tume ya Ushindani (FCC) imefanya semina wezeshi kwa wafanyabiashara wa pikipiki na spea zake jijini Dar es Salaam Februari 26, 2018.
 
Semina hiyo iliyohudhuriwa na wawakilishi takriban 30 wakiwemo viongozi wa Chama cha Wafanyabiashara hao, CHAWASAPI, pamoja na wafanyabiashara wa pikipiki na spea zake, ilifunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji Uwekezaji katika Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Leo Lyayuka.
 
Akifungua semina hiyo alibainisha kuwa jukumu la FCC ni sawa na mwamuzi wa kati katika mpira wa miguu na chombo hicho kimeamua kuwapatia elimu ili kuongezea nguvu eneo la utekelezaji sharia.
 
Mada mbalimbali ziliwasilishwa katika semina hiyo na wafanyabiashara hao kwa ujumla waliishukuru na kuipongeza FCC kwa kuendesha semina hiyo wezeshi. Aidha, waliishauri Tume kuongeza upelekaji wa semina za aina hiyo kwa wafanyabiashara waliopo mikoani ili kuwawezesha wafanyabiashara kuwa wadau muhimu katika ukuaji wa uchumi.