TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
FCC Yaridhia
Maombi Matatu ya Miungano ya Kampuni
Kwa mujibu wa kanuni Namba 42(13)
ya Kanuni za Utendaji za Tume ya Ushindani za mwaka 2013, Tume ya ushindani
imeridhia bila masharti, maombi matatu ya miungano ya kampuni katika kikao
chake cha 55 cha mashauri ya ushindani kilichofanyika Aprili 17, 2014. Maombi
hayo yaliwasilishwa katika ofisi za Tume kati ya Desemba 20 ,2013 na Machi 28,
2014 na kampuni zilizokuwa zikikusudia kutekeleza makubaliano ya miungano hiyo.
Miungano iliyoridhiwa na Tume ni
kama ifuatavyo:
S/N.
|
Kampuni Inayonunua
|
Kampuni Iliyolengwa Kuhusishwa
|
1.
|
AVIS Southern Africa
|
Tanzuk Limited
|
2.
|
Vodacom Group Limited
|
Cavalry Holdings Limited
|
3.
|
Dutch Oak Tree Foundation
|
Tanga Dairies Cooperative Union
na Tanga Fresh Limited
|
Muungano baina ya kampuni za AVIS
Southern Africa na Tanzuk Limited unahusisha biashara za ukodishaji wa magari
pamoja na huduma zinazoambatana nazo. Muungano baina ya kampuni za Vodacom
Group Limited na Cavalry Holdings Limited unahusiana na huduma za mawasiliano
ya simu, wakati muungano baina ya kampuni za Dutch Oak Tree Foundation na Tanga
Dairies Cooperative Union and Tanga Fresh Limited unahusisha sekta ya biashara
ya maziwa.
Katika kuhakikisha kuwa sheria
inafuatwa, kampuni ya Dutch Oak Tree Foundation iliwasilisha katika Tume
taarifa ya kuungana na Tanga Dairies Cooperative Union na Tanga Fresh Limited
tarehe 20 Decemba, 2013. Taarifa ya muungano baina ya kampuni za AVIS
Southern Africa na Tanzuk Limited ilitolewa katika Tume tarehe 21 Machi, 2014.
Muungano baina ya Vodacom Group Limited na Cavalry Holdings Limited ulitolewa
taarifa katika Tume tarehe 28, Machi, 2014. Taarifa za miungano yote zilitolewa
ka mujibu wa kipengele cha 11(2) cha Sheria ya Ushindani (Na. 8 ya mwaka 2003)
na Kanuni ya 33(1) ya Kanuni za Utendaji za tume za mwaka 2013.
Tume iliridhia miungano hiyo ya
kampuni baada ya kukamilisha tathmini ya maombi husika kuanzia hatua ya awali
ya utoaji wa taarifa na kuridhika kuwa miungano hiyo, endapo itaruhusiwa
kuendelea, haitaathiri ushindani kwa mujibu wa kipengele cha 11(1) cha Sheria
ya Uhsindani (FCA) na kanuni za utendaji za Tume za mwaka 2013. Baada ya
kuzingatia taarifa ya maombi ya kuungana kwa kampuni husika kwa mujibu wa
Sheria, Tume iliridhika kuwa miungano hiyo haijakinzana na Sheria ya Ushindani
(Na. 8 ya mwaka 2003).
Kati ya Julai 1, 2013 na Machi 28, 2014, FCC iliridhia
jumla ya maombi ishirini na moja (21) ya miungano ya kampuni iliyotolewa
taarifa na kuwasilishwa kwa tathmini katika Tume, yakiwemo maombi ya miungano
mitatu iliyoainishwa hapo juu. Maombi mengine ya miungano yaliyoridhiwa na Tume
ni pamoja na: InReturn East Africa Fund I.C.V na
Dar es Salaam Corridor Group Limited; SCPE, CSSAF & PRIF Afrivest naETC Group
(Mauritius) Limited; Apollo Acquisition Corp na Cooper
Tire & Rubber Company; Prime Bank Ltd, First Merchant Bank na Premier Capital Mauritius Ltd and
International Commercial Bank; HTT
Infraco Ltd na Vodacom Tanzania
Limited; TransUnion Africa Holdings Proprietary Ltd na Credit Reference Bureau
(Holdings) Ltd; pamoja na EFFCO
Solutions (T) Ltd na EFFCO (Proprietary)
Ltd.
Miungano mingine iliyoridhiwa ni baina ya MMG Exploration Holdings Ltd na IMX
Resources Ltd; Untrac Holding Ltd na Delta Holding Group; Mauritius Union Assurance Cy Ltd na Phoenix Transafrica
Holdings Ltd; Petrobas Oil &
Gas B.V na Petrobas Tanzania Ltd; State Mining Corporation (STAMICO) and ABG
Exploration Limited; State Mining Corporation (STAMICO) na Pangea Minerals
Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited na Ophir East Africa
Holdings Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited na Mzalendo Gas
Processing Company Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited na Ruvuma
Pipeline Company Limited; Al Futtaim Autom & Machinery Company LLC na Hughes
Motors (Tanzania) Limited; Al Futtaim Autom & Machinery Company LLC na
Hughes Agricultural (Tanzania) Limited.
Kipengele cha 11(2)
cha Sheria ya Ushindani (Na. 8 ya mwaka 2003) pamoja na Kanuni za Kizingiti cha
Utangazaji wa Miungano ya Kampuni za mwaka 2007, kama zilivyorekebishwa na
Notisi ya Serikali Namba 93 ya Aprili
17, 2009, zinabainisha kuwa kampuni zote ambazo thamani ya pamoja ya rasilimali
zake au mapato yake ya mwaka yanazidi Sh. Milioni 800 zinapaswa kuiarifu Tume
kabla ya kuanza kutekeleza makubaliano ya kuungana.
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma.
Mei 3,
2014
No comments:
Post a Comment