
This Blog keeps you abreast key events relating to the Fair Competition Commission. The Commission was established by the Fair Competition Act (No. 8 of 2003) to promote and protect effective competition in Trade and Commerce and to protect consumers from misleading and deceptive conducts. It also fights counterfeits under the Merchandise Marks Act (1963) as amended.
Sunday, 4 May 2014
FCC Yaridhia Maombi ya Kampuni Kuungana
TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
FCC Yaridhia
Maombi Matatu ya Miungano ya Kampuni
Kwa mujibu wa kanuni Namba 42(13)
ya Kanuni za Utendaji za Tume ya Ushindani za mwaka 2013, Tume ya ushindani
imeridhia bila masharti, maombi matatu ya miungano ya kampuni katika kikao
chake cha 55 cha mashauri ya ushindani kilichofanyika Aprili 17, 2014. Maombi
hayo yaliwasilishwa katika ofisi za Tume kati ya Desemba 20 ,2013 na Machi 28,
2014 na kampuni zilizokuwa zikikusudia kutekeleza makubaliano ya miungano hiyo.
Miungano iliyoridhiwa na Tume ni
kama ifuatavyo:
S/N.
|
Kampuni Inayonunua
|
Kampuni Iliyolengwa Kuhusishwa
|
1.
|
AVIS Southern Africa
|
Tanzuk Limited
|
2.
|
Vodacom Group Limited
|
Cavalry Holdings Limited
|
3.
|
Dutch Oak Tree Foundation
|
Tanga Dairies Cooperative Union
na Tanga Fresh Limited
|
Muungano baina ya kampuni za AVIS
Southern Africa na Tanzuk Limited unahusisha biashara za ukodishaji wa magari
pamoja na huduma zinazoambatana nazo. Muungano baina ya kampuni za Vodacom
Group Limited na Cavalry Holdings Limited unahusiana na huduma za mawasiliano
ya simu, wakati muungano baina ya kampuni za Dutch Oak Tree Foundation na Tanga
Dairies Cooperative Union and Tanga Fresh Limited unahusisha sekta ya biashara
ya maziwa.
Katika kuhakikisha kuwa sheria
inafuatwa, kampuni ya Dutch Oak Tree Foundation iliwasilisha katika Tume
taarifa ya kuungana na Tanga Dairies Cooperative Union na Tanga Fresh Limited
tarehe 20 Decemba, 2013. Taarifa ya muungano baina ya kampuni za AVIS
Southern Africa na Tanzuk Limited ilitolewa katika Tume tarehe 21 Machi, 2014.
Muungano baina ya Vodacom Group Limited na Cavalry Holdings Limited ulitolewa
taarifa katika Tume tarehe 28, Machi, 2014. Taarifa za miungano yote zilitolewa
ka mujibu wa kipengele cha 11(2) cha Sheria ya Ushindani (Na. 8 ya mwaka 2003)
na Kanuni ya 33(1) ya Kanuni za Utendaji za tume za mwaka 2013.
Tume iliridhia miungano hiyo ya
kampuni baada ya kukamilisha tathmini ya maombi husika kuanzia hatua ya awali
ya utoaji wa taarifa na kuridhika kuwa miungano hiyo, endapo itaruhusiwa
kuendelea, haitaathiri ushindani kwa mujibu wa kipengele cha 11(1) cha Sheria
ya Uhsindani (FCA) na kanuni za utendaji za Tume za mwaka 2013. Baada ya
kuzingatia taarifa ya maombi ya kuungana kwa kampuni husika kwa mujibu wa
Sheria, Tume iliridhika kuwa miungano hiyo haijakinzana na Sheria ya Ushindani
(Na. 8 ya mwaka 2003).
Kati ya Julai 1, 2013 na Machi 28, 2014, FCC iliridhia
jumla ya maombi ishirini na moja (21) ya miungano ya kampuni iliyotolewa
taarifa na kuwasilishwa kwa tathmini katika Tume, yakiwemo maombi ya miungano
mitatu iliyoainishwa hapo juu. Maombi mengine ya miungano yaliyoridhiwa na Tume
ni pamoja na: InReturn East Africa Fund I.C.V na
Dar es Salaam Corridor Group Limited; SCPE, CSSAF & PRIF Afrivest naETC Group
(Mauritius) Limited; Apollo Acquisition Corp na Cooper
Tire & Rubber Company; Prime Bank Ltd, First Merchant Bank na Premier Capital Mauritius Ltd and
International Commercial Bank; HTT
Infraco Ltd na Vodacom Tanzania
Limited; TransUnion Africa Holdings Proprietary Ltd na Credit Reference Bureau
(Holdings) Ltd; pamoja na EFFCO
Solutions (T) Ltd na EFFCO (Proprietary)
Ltd.
Miungano mingine iliyoridhiwa ni baina ya MMG Exploration Holdings Ltd na IMX
Resources Ltd; Untrac Holding Ltd na Delta Holding Group; Mauritius Union Assurance Cy Ltd na Phoenix Transafrica
Holdings Ltd; Petrobas Oil &
Gas B.V na Petrobas Tanzania Ltd; State Mining Corporation (STAMICO) and ABG
Exploration Limited; State Mining Corporation (STAMICO) na Pangea Minerals
Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited na Ophir East Africa
Holdings Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited na Mzalendo Gas
Processing Company Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited na Ruvuma
Pipeline Company Limited; Al Futtaim Autom & Machinery Company LLC na Hughes
Motors (Tanzania) Limited; Al Futtaim Autom & Machinery Company LLC na
Hughes Agricultural (Tanzania) Limited.
Kipengele cha 11(2)
cha Sheria ya Ushindani (Na. 8 ya mwaka 2003) pamoja na Kanuni za Kizingiti cha
Utangazaji wa Miungano ya Kampuni za mwaka 2007, kama zilivyorekebishwa na
Notisi ya Serikali Namba 93 ya Aprili
17, 2009, zinabainisha kuwa kampuni zote ambazo thamani ya pamoja ya rasilimali
zake au mapato yake ya mwaka yanazidi Sh. Milioni 800 zinapaswa kuiarifu Tume
kabla ya kuanza kutekeleza makubaliano ya kuungana.
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma.
Mei 3,
2014
FCC Approves Three Merger Applications
FCC Approves
Three Merger Applications
The Fair Competition Commission
had in its 55th Case Hearing Meeting held on 17th April,
2014, acting pursuant to Rule 42(13) of the Fair Competition Procedural Rules
2013, approved without conditions three merger applications notified at the
Commission by the merging parties between 20th December, 2013 and 28th
March, 2014.
The approved mergers are as
follows:
S/N.
|
Acquiring Firm
|
Target Firm
|
1..
|
AVIS Southern Africa
|
Tanzuk Limited
|
2.
|
Vodacom Group Limited
|
Cavalry Holdings Limited
|
3.
|
Dutch Oak Tree Foundation
|
Tanga Dairies Cooperative Union
and Tanga Fresh Limited
|
The Merger between AVIS Southern
Africa and Tanzuk Limited relate to automotive leasing business focusing on
products, services, research trends and industry insight by the leasing
experts.
The Merger between Vodacom Group
Limited and Cavalry Holdings Limited relates o the telecommunications service
industry, whereas the merger between Dutch Oak Tree Foundation and Tanga
Dairies Cooperative Union and Tanga Fresh Limited takes place in the dairy
industry.
A merger application between
Dutch Oak Tree Foundation and Tanga Dairies Cooperative Union and Tanga Fresh
Limited was notified at the Commission on 20th December, 2013. A
merger application between AVIS Southern Africa and Tanzuk Limited was notified
at the Commission on 21st March, 2014 whereas that between Vodacom
Group Limited and Cavalry Holdings Limited was notified on 28th
March, 2014. All notifications were made pursuant to Section 11(2) of the Fair
Competition Act (No. 8 of 2003) and Rule 33(1) of the Fair Competition
Procedural Rules, 2013.
The approvals were granted after
FCC had gone through evaluation of notified merger applications at all stages
and becoming satisfied that the transactions were not likely to harm
competition according to section 11(1) of the Fair Competition Act and the Fair
Competition Procedural Rules, 2013. After considering the parties’ submissions
and provisions of the law; the Commission determined that the intended merger
did not breach the provisions of the Fair Competition Act, No. 8 of 2003.
Between 1st July, 2013 and 28th
March, 2014, FCC had approved a total of twenty one (21) notified merger
applications without conditions, including the three mentioned above. Other
approved notified merger applications in that timeline include the following: InReturn
East Africa Fund I.C.V and
Dar es Salaam Corridor Group Limited; SCPE, CSSAF & PRIF Afrivest and ETC Group
(Mauritius) Limited; Apollo Acquisition Corp and Cooper
Tire & Rubber Company; Prime Bank Ltd, First Merchant Bank and Premier Capital Mauritius Ltd and
International Commercial Bank; HTT
Infraco Ltd and Vodacom Tanzania
Limited; TransUnion Africa Holdings Proprietary Ltd and Credit Reference Bureau
(Holdings) Ltd; and EFFCO Solutions (T) Ltd and EFFCO (Proprietary) Ltd.
Other approved mergers are those between MMG Exploration Holdings Ltd and IMX
Resources Ltd; Untrac Holding Ltd and Delta Holding Group; Mauritius Union Assurance Cy Ltd and Phoenix Transafrica
Holdings Ltd; Petrobas Oil &
Gas B.V and Petrobas Tanzania Ltd; State Mining Corporation (STAMICO) and ABG
Exploration Limited; State Mining Corporation (STAMICO) and Pangea Minerals
Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited and Ophir East Africa
Holdings Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited and Mzalendo Gas
Processing Company Limited; Pavilion Strategic Holdings 1 Pte Limited and
Ruvuma Pipeline Company Limited; Al Futtaim Autom & Machinery Company LLC
and Hughes Motors (Tanzania) Limited; Al Futtaim Autom & Machinery Company
LLC and Hughes Agricultural (Tanzania) Limited.
Section 11(2) of the
Fair Competition Act (No. 8 of 2003) and the Fair Competition (Threshold
Notification of a Merger) Order, 2007, as amended by GN No. 93 of 17th
April, 2009 points out that firms should notify a merger to the Commission if
the combined value of assets or turnover reaches the set threshold of TShs 800
million.
Issued by the
Communications and Public Relations Unit
3rd
May, 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)